UMDHANIAYE NDIYE SIYE

Adui mpende ila usimtende. Yule umdhaniaye ndiye rafiki huenda akawa mnafiki. Akose kukufaa hata siku ya dhiki.

Dunia ni mviringo Kuna wale wanyenyekevu na wenye maringo. Yaruhusu majira magumu. Kukuashiria wale wa kudumu.

Yule rafiki wa maishani Huenda akakuacha ukiwa mashakani. Na asijawe na huruma tumaini lako likipukutika kama majani

Wakati mwingine familia zimegeukana. Pasiwe na yeyote aliye na ari ya kusaidiana. Mara ngapi tumeskia baba kampokonya mwanawe mchumba? Tamaa ishamfanya kumkosea heshima muumba.

Wengine wetu machozi tumepanguzwa na tusiowajua. Chakula tukalishwa na tusiowatambua. Na wakati mwingine tumaini la kupona tukapewa na wanaougua. Kwani wewe hujaskia kikulacho ki nguoni mwako?

About the Author

Leave a Reply

You may also like these

No Related Post

error: Content is protected !!

Discover more from Osprey Empire

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading