Kilio Moyoni

Miaka na mikaka

Ulimwengu nmetembea

Viatu vyaweza nena

Milima na mabonde nimepitia

Miaka na mikaka

Nyumbani kutamu

Utamu wa kukaa bure

Ila chakula hakuna

Mikono tumenawa

Mara mia kwa siku

Ila tumboni hakuna

Kunawa mikono bila lishe Kuna haja gani?

Kila siku nitembeapo

Kartasi za kazi nimebeba mfukoni

Barua za kuomba kazi nimeandika na kutuma ofisi mbalimbali

Lakini hakuna jibu kamwe

Kazi nimetafuta kwa miaka mingi

Ili watoto wapate karo,chakula na malazi

Mahitaji nyumbani chungu nzima

Kazi hakuna, chakula hakuna

Ndugu zangu wanitegemea

Ndiposa niwatimizie mahitaji yao

Kilio cha huzuni

Kimekunja nyuso zao

Fikra zimeniadama

Miba ya umaskini imedunga maisha yetu

Machozi ya damu yametiririka hadi moyoni

Kazi hakuna,pesa hakuna, nyumbani hakuna chakula …ni kilio tu ,,jameni tufanyeje??

@Januaris Musyoka

About the Author

Leave a Reply

You may also like these

error: Content is protected !!

Discover more from Osprey Empire

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading